Wakaomboleza, wakalia na kufunga kula mpaka magaribi kwa ajili ya Saulo, Yonatani mwana wake, na inchi ya Waisraeli, watu wa Yawe, kwa maana wengi kati yao waliuawa katika vita.
Kisha, watu wote walikwenda kumusihi Daudi akule chakula wakati ulipokuwa bado muchana. Lakini Daudi aliapa akawaambia: “Mungu aniue ikiwa nitaonja chakula au kitu chochote mpaka jua litakapotua.”
Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia, ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia. Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu, na kutenda uovu mukubwa.
Wafilistini wakamukamata, wakamwongoa macho, wakamupeleka Gaza, wakamufunga kwa minyororo ya shaba, na kumulazimisha kufanya kazi ya kusaga unga kule katika kifungo.