Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 24:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Halafu, mufalme akamwambia Yoabu na majemadari wa kundi la waaskari waliokuwa pamoja naye: “Muzunguke katika makabila yote ya Waisraeli kutokea Dani mpaka Beri-Seba, muwahesabu watu kusudi nipate kujua jumla yao.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 24:2
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.


Shauri langu ni kwamba uwakusanye kwako watu wote wa Israeli tangia Dani mpaka Beri-Seba wakuwe wengi kama muchanga wa bahari, na wewe mwenyewe peke yako uende kwa vita.


Yoabu mwana wa Zeruya na watumishi wengine wa Daudi, nao walitoka na kukutana na Abeneri na watu aliokuwa nao kwenye kiziwa kinachokuwa kule Gibeoni. Kikundi kimoja kikajipanga upande mumoja wa kiziwa na kingine upande mwingine.


Sasa Yoabu alikuwa jemadari wa waaskari wote wa Waisraeli. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa Wakereti na Wapeleti.


Zeleki wa inchi ya Waamoni; Naharayi wa muji Beroti aliyekuwa mubebaji wa silaha wa Yoabu mwana wa Zeruya;


Basi, Yawe akawaletea Waisraeli ugonjwa, tangu asubui mpaka wakati uliopangwa. Watu elfu makumi saba walikufa katika inchi yote kutoka Dani mpaka Beri-Seba.


Yawe alimwapia Daudi kwamba atauhamisha ufalme kutoka jamaa ya Saulo na kumupa yeye. Naye atatawala inchi ya Israeli na Yuda kutokea Dani mpaka Beri-Seba.”


Yoabu mwana wa Zeruya alikuwa jemadari wa makundi yake ya waaskari. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari za kifalme.


Halafu, Daudi akamwambia Yoabu na wale majemadari wengine: “Mwende muwahesabu Waisraeli, kutokea Beri-Seba mpaka Dani. Muniletee habari kusudi nijue hesabu yao.”


na hata wakati ambapo wajumbe wa wakubwa wa Babeli waliotumwa kwake kuuliza juu ya mambo ya ajabu yaliyotokea mule, Mungu, alimwacha ajiamulie mwenyewe, kusudi amupime na kujua yote yaliyokuwa ndani ya moyo wake.


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.


Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.


Watu wote wa Israeli, kutokea Dani mpaka Beri-Seba, pamoja na watu wa inchi ya Gileadi, wakakusanyika kule Misipa, mbele ya Yawe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις