2 Samweli 23:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200231 Abialboni wa muji Araba; Azimaweti wa muji Bahurimu; Δείτε το κεφάλαιο |
Kiongozi wao alikuwa Ahiezeri aliyesaidiwa na Yoasi, wote wawili ni wana wa Sema kutoka Gibea, Yezieli na Peleti, wana wa Azimaweti, Beraka na Yehu kutoka Anatoti, Isimaya kutoka Gibeoni aliyekuwa mutu shujaa kati ya wale makumi tatu na kiongozi wao, Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi kutoka Gedera, Elizai, Yeremoti, Bealia, Semaria, na Sefatia wa muji wa Harufi, Elekana, Isia, Azareli, Yoezeri, Yasobeamu kutoka ukoo wa Kora, Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
Hawa ni wasimamizi wa mali ya mufalme Daudi: Azimaweti mwana wa Adieli alisimamia hazina za mufalme Daudi. Yonatani mwana wa Usia alisimamia hazina zilizokuwa katika inchi, miji, vijiji na katika minara. Ezeri mwana wa Kalebu alisimamia walimaji. Simei wa muji wa Ramati alisimamia kazi ya mashamba ya mizabibu. Zabudi wa muji wa Sifi alisimamia mazao ya mashamba ya mizabibu. Bali-Hanani wa muji wa Gederi alisimamia mizabibu na mikuyu ya inchi ya Shefela. Yoasi alisimamia gala za mafuta. Sitirayi wa muji wa Saroni alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa kule Sarani. Safati wa muji wa Adilai alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa katika mabonde. Obili Mwisimaeli alisimamia ngamia. Yedeya, Mumeronoti alisimamia punda dike. Yasisi, Muhagri, alisimamia makundi ya kondoo.