Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 23:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 23:3
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Basi, akajenga mazabahu pahali pale na kuiita “Mungu ni Mungu wa Israeli”.


Nani anayekuwa Mungu isipokuwa Yawe? Nani anayekuwa kikingio isipokuwa Mungu wetu?


Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Tangu wakati nilipochaguliwa kuwa mutawala wa inchi ya Yuda kwa miaka kumi na miwili ni kusema tangu mwaka wa makumi mbili mpaka mwaka wa makumi tatu na mbili wa utawala kwa mufalme Artasasta, sikukula chakula kinachostahili kukuliwa na mutawala, wala wandugu zangu hawakufanya hivyo.


Anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki? Utasubutu kumuhukumu mwenye haki na mwenye nguvu,


Yawe ataeneza mamlaka yako kutoka Sayuni; utatawala juu ya waadui zako wote.


Yawe atanijalia wema wake muchana; nami nitamwimbia wimbo wa sifa usiku, nitamwomba Mungu anayenipa uzima.


Zaburi ya Solomono. Ee Mungu, umujalie mufalme uwezo wa kufuata sheria yako, umupe mwana wa mufalme haki yako.


Atawale taifa lako kwa haki, na wamasikini wako kwa sheria yako.


Lakini juu ya mambo mengine, chagua kati ya watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomwogopa Mungu, waaminifu na wanaochukia kituliro. Uwape hao mamlaka, wakuwe na kazi ya kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, makumi tano na kumikumi.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Yawe, Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutuma kwao. Hili ndilo jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote.


Sema kwa ajili yao na kuamua kwa haki, linda haki za wamasikini na wakosefu.


Kutatokea mufalme atakayetawala kwa haki, nao wakubwa wataongoza kwa kufuatana na sheria ya Mungu.


Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Lakini juu ya Mwana, Mungu alisema: “Kiti chako cha kifalme, Ee Mungu, kitadumu hata milele. Unatawala ufalme wako kwa haki.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις