walimwendea Gedalia kule Misipa. Watu hao walikuwa Isimaeli mwana wa Netania, Yohana na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanumeti, nao wana wa Efai kutoka muji Netofa, na Yezania wa muji wa Makati; wote pamoja na watu wao.
Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.