37 Umepanua njia yangu wala miguu yangu haikuteleza.
Alinileta, akaniweka kwenye nafasi ya usalama; aliniponyesha kwa sababu alipendezwa nami.
Hatakuacha uanguke; mulinzi wako hasinzii.
Nimefuata siku zote njia yako; wala sijatereza hata kidogo.
Umenipa ngao yako ya wokovu na kuniimarisha kwa mukono wako wa kuume. Nimefanikiwa kwa sababu ulikubali kunisaidia.
Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Daudi.
Nilipotambua kwamba ninateleza, wema wako, ee Yawe, ulinikingia.
Ukitembea hatua zako hazitazuizwa, wala ukikimbia hautajikwaa.
Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.