Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Watu wa Yuda walimwendea Daudi kule Hebroni wakamupakaa mafuta akuwe mufalme wao. Daudi aliposikia kwamba watu wa Yabesi-Gileadi ndio waliomuzika Saulo,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 2:4
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Tena Abusaloma ambaye tulimupakaa mafuta akuwe mufalme wetu, sasa ameuawa katika vita. Sasa, kwa nini hatuzungumuzii juu ya kumurudisha mufalme Daudi?”


Kisha, watu wote wa Israeli wakakuja kwa mufalme na kumwambia: “Kwa nini wandugu zetu watu wa Yuda walikuwa wamekutwaa ukiwa katika njia, wakakuvukisha muto Yordani, wewe na jamaa yako, pamoja na watu wako?”


Daudi alikuwa mufalme wa kabila la Yuda kwa muda wa miaka saba na nusu, makao yake yalikuwa kule Hebroni.


Lakini mukuwe imara na mashujaa. Saulo, bwana wenu, amekufa, na watu wa Yuda wamenipakaa mafuta nikuwe mufalme wao.”


Daudi alisikia yale Risipa binti ya Aya, habara ya Saulo aliyofanya.


Alikwenda na kuitwaa mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani kutoka kwa wakaaji wa Yabeshi-Gileadi, waliokuwa wameiiba kutoka kule Beti-Sani, ambako Wafilistini walikuwa wamemutundika Saulo na Yonatani siku ile walipomwua Saulo kwenye mulima Gilboa.


Wafilistini waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mufalme wa Waisraeli, wote walitoka kwenda kumutafuta, lakini yeye alipata habari, akaingia ndani ya makimbilio.


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.


Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.


Halafu Yehoyada akamutoa inje mwana wa mufalme, akamuvalisha taji juu ya kichwa, na kumupa maandiko ya sheria. Wakamuweka kuwa mufalme na kumupakaa mafuta. Wakapiga mikono na kusema: “Mufalme aishi milele!”


Lakini watu wa Yebesi Gileadi waliposikia yote Wafilistini waliyomutendea Saulo,


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme kule Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Waisraeli kulingana na neno la Yawe lililotolewa kwa njia ya Samweli.


Siku kwa siku, watu walijiunga na Daudi kwa kumusaidia, na nyuma akakuwa na kundi kubwa sana la waaskari, kama jeshi la Mungu.


Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις