Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 19:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sasa, simama uzungumuze na watumishi wako kwa upole. Maana, ninaapa kwa Yawe, kama hauendi kuzungumuza nao, hakuna hata mumoja atakayebaki pamoja nawe leo magaribi. Hili litakuwa jambo baya zaidi kwako kuliko maovu yote yaliyokupata tangu ujana wako mpaka leo.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 19:8
10 Σταυροειδείς Αναφορές  

Abusaloma alizoea kuamuka asubui mapema na kwenda kusimama kwenye njia inayoelekea kwenye mulango wa muji. Mutu yeyote aliyekuwa na mashitaki ambayo alitaka kuyapeleka kwa mufalme kwa kupata uamuzi wake, Abusaloma alimwita mutu yule pembeni na kumwuliza: “Unatoka katika muji gani?” Kama mutu yule akisema ametoka katika muji fulani wa kabila la Waisraeli,


Wakamukamata Abusaloma, wakamutupia ndani ya shimo kubwa katika pori na kulundika lundo kubwa sana la mawe juu yake. Watu wote wa Israeli wakakimbia, kila mumoja kwake.


Daudi alikuwa ameikaa kati ya milango miwili ya muji. Naye mulinzi wa mulango akapanda juu ya ukuta mpaka juu ya mulango na alipoinua macho yake aliona mutu akikimbia peke yake.


Mufalme akawaambia: “Nitafanya sawa vile munavyoona kuwa vizuri.” Kwa hiyo, mufalme akasimama pembeni ya mulango, nao waaskari wake wakipita: mamia na maelfu.


Ushindi wa siku hiyo uligeuzwa kuwa maombolezo kwa watu wote, waliposikia kwamba mufalme anamwombolezea Abusaloma.


Jua liliposhuka, amri ikatolewa: “Kila mutu arudie kwake! Kila mutu arudie kwake!”


Watu wa Yuda walishindwa na watu wa Israeli na kila mumoja alirudi kwake.


Kwa hiyo Yoramu aliondoka na magari yake yote kwenda Sairi. Wakati wa usiku alitoka na waongozi wake wa magari akawashambulia Waedomu waliokuwa wamemuzunguka. Lakini waaskari wake walikimbilia kwao.


Wafilistini walipiga vita, na Waisraeli walishindwa na kukimbia kila mutu kwake. Siku hiyo kulikuwa mauaji makubwa maana waaskari wa miguu elfu makumi tatu wa Israeli waliuawa.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις