Lakini Daudi aliendelea, akapanda kwenye mulima wa Mizeituni akilia, bila viatu na kichwa chake kimefunikwa. Hata watu wote waliokuwa pamoja naye walifunika vichwa vyao, wakapanda mulima wakilia.
Wakamukamata Abusaloma, wakamutupia ndani ya shimo kubwa katika pori na kulundika lundo kubwa sana la mawe juu yake. Watu wote wa Israeli wakakimbia, kila mumoja kwake.
Halafu Yoabu aliingia katika nyumba ya mufalme, akamwambia: “Leo umetupatisha haya sisi watumishi wako wote ambao leo tumeyaokoa maisha yako, maisha ya watoto wako wanaume, na maisha ya watoto wako wanawake, maisha ya wake zako na maisha ya wahabara zako.
Ijapokuwa mumenipakaa mafuta kusudi nikuwe mufalme, lakini leo mimi ni zaifu. Hawa wana wa Zeruya ni wakali kupita kipimo. Yawe awaazibu waovu hawa sawasawa na uovu wao.”
Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.