Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 19:43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

43 Watu wa Yuda wakawaambia watu wa Israeli: “Kwa sababu mufalme ni ndugu yetu wa karibu. Kwa nini munakasirika juu ya jambo hili? Tumekula nini wakati wowote kutoka kwake? Au yeye ametupatia zawadi yoyote?”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 19:43
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

Muulize vilevile Amasa kama yeye si damu yangu. Tena Mungu aniue ikiwa simufanyi yeye kuwa jemadari wa kundi langu la waaskari tangu leo pahali pa Yoabu.’ ”


Kisha, mufalme akatoka, akaenda, akaikaa kwenye nafasi yake karibu na mulango. Watu wote walipoambiwa kwamba mufalme yuko kwenye mulango, wote walimwendea. Wakati ule, watu wote wa Israeli walikuwa wamekimbia, kila mumoja kwake.


Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Daudi akamwambia Abisayi: “Sasa, Seba mwana wa Bikiri, atatuletea taabu kuliko Abusaloma. Twaa watumishi wangu, umufuate Seba kusudi asiingie kwenye miji yenye kuta na kuponyoka tusimwone tena.”


Kisha makabila yote ya Waisraeli yalimwendea Daudi kule Hebroni, na kumwambia: “Angalia, sisi ni mwili na damu yako.


Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali, walimwambia: “Hatuna ushirika wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Murudie kwenu, enyi watu wa Israeli! Uitunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi kila mutu kwake.


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.


Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.


Ndugu aliyetendewa kosa ni mugumu kuliko muji wenye ukuta; magomvi yanakaza kama vile vifungio vya mulango wa ukuta.


Usijiachilie kushindwa na ubaya, lakini ushinde ubaya kwa kutenda mema.


Lakini kama mukiumana na kukulana kama nyama wa pori, muangalie vizuri musiteketezane.


kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,


Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.


Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.


Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.


Watu wa kabila la Efuraimu wakamwuliza Gideoni: “Kwa nini umetutendea hivyo? Kwa nini haukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakamugombeza kwa ukali.


Kisha Mungu akaleta roho ya uadui kati ya Abimeleki na watu wa Sekemu, nao wakamwasi.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις