3 Ushindi wa siku hiyo uligeuzwa kuwa maombolezo kwa watu wote, waliposikia kwamba mufalme anamwombolezea Abusaloma.
Kwa nini ulitoroka kwa siri, ukanidanganya, wala haukuniarifu kusudi nipate kukuaga kwa shangwe, nyimbo, matari na vinubi?
Basi, Daudi akaenda Mahanaimu. Abusaloma akavuka muto Yordani na watu wote wa Israeli.
Yoabu alipata habari kwamba mufalme alikuwa akilia na kuomboleza juu ya kifo cha Abusaloma.
Barzilayi wa Gileadi alikuwa amefika kutoka Rogelimu. Alikuwa amekwenda pamoja na mufalme kwenye muto Yordani kwa kumusindikiza mpaka ngambo ya muto.
Kwa hiyo, siku hiyo, watu waliingia katika muji kimyakimya kama watu wanaorudi katika muji wakipata haya kwa kukimbia vita.