2 Samweli 18:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Yoabu akamwambia mutu yule: “Nini? Ulimwona Abusaloma? Kwa nini, basi, haukumupiga na kumwua palepale? Ningefurahi kukulipa vikoroti kumi vya feza na mukaba.”
Lakini yule mutu akamwambia Yoabu: “Hata kama ningeuona uzito wa vikoroti elfu moja vya feza katika mukono wangu, singeunyoosha mukono wangu juu ya mwana wa mufalme kwa kumwua. Maana, tulimusikia mufalme alipokuamuru wewe Abisayi na Itayi, kwamba kwa ajili yake, mumulinde kijana Abusaloma.