Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 17:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 17:14
25 Σταυροειδείς Αναφορές  

Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Wakati ule, Daudi aliambiwa kwamba hata Ahitofeli alikuwa mumoja wa waasi waliojiunga na Abusaloma. Lakini Daudi akaomba akisema: “Ee Yawe, ninakuomba uyafanye mashauri ya Ahitofeli yasifanikiwe.”


Urudi Yerusalema na kumwambia Abusaloma: ‘Nitakuwa mutumishi wako, ee mufalme, kama vile nilivyokuwa zamani mutumishi wa baba yako’. Kwa njia hiyo utanisaidia kupinga mashauri ya Ahitofeli.


Siku hizo, shauri lolote Ahitofeli alilotoa lilikuwa kama limetolewa na Mungu. Na shauri la Ahitofeli liliheshimiwa na Daudi na Abusaloma.


Halafu mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Mungu kusudi Yawe atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu, mwana wa Nebati kwa njia ya Ahiya wa Shilo.


Lakini Rehoboamu alizarau shauri la wazee na kwa pahali pake akashauriana na vijana waliokomaa pamoja naye ambao walikuwa washauri wake.


Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Lakini Amazia hakujali kwa maana lilikuwa kusudi la Mungu apate kuwekwa katika mukono wa waadui zao kwa sababu alitegemea miungu ya Edomu.


Hivyo, tukaendelea kufanya kazi yetu na nusu ya watu wakishika silaha tangu mapambazuko mpaka nyota zinapoonekana mbinguni.


Anawatembeza washauri miguu wazi, anawafanya waamuzi kuwa wapumbafu.


kusudi nitangaze sifa zako mbele ya watu wa Sayuni, nipate kushangilia kwa sababu umeniokoa.


Mataifa yameanguka katika shimo walilochimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliotega.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


Nani anayeweza kusema kusudi kitu kifanyike ikiwa Yawe asipoamuru ikuwe hivyo?


Hata wakijificha juu ya mulima Karmeli, huko nitawatafuta na kuwakamata; hata wakijificha mbali nami katika vilindi vya bahari, mule nitaiamuru nyoka kubwa ya bahari iwaume.


Basi bwana wa yule mulinzi akamusifu kwa sababu alitenda kwa werevu. Kwa maana watu wa dunia hii wanatengeneza maneno yao na wenzao kwa werevu sana kuliko watu wanaopenda kuishi katika mwangaza.”


Kwa maana hekima ya kidunia ni upumbafu mbele ya Mungu. Ni sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mungu anawanasa wenye hekima katika werevu wao wenyewe.”


“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις