Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 17:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Watu wako watakaposikia hivyo, hata wale ambao ni hodari, wenye mioyo kama ya simba, watavunjika kabisa moyo kwa woga. Maana, Waisraeli wote wanajua kwamba baba yako ni shujaa na wote wanaokuwa pamoja naye ni watu hodari.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 17:10
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wewe Yuda, mwana wangu, ni kama mwana-simba ambaye amepata mawindo yake akapanda juu, kama simba mukali anajinyoosha na kulala chini. Simba dike, nani anayesubutu kumwamusha?


Saulo na Yonatani, watu wema na wa kupendeza. Katika maisha na kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, wenye nguvu kuliko simba.


Hata sasa amekwisha kujificha katika pango moja au nafasi ingine. Ikiwa tu katika mashambulizi ya mwanzo kunakufa watu kati yetu, habari itasambaa kwamba wafuasi wa Abusaloma wameshindwa vibaya.


Naye Benaya mwana wa Yehoyada wa muji Kabuseli, alikuwa askari shujaa ambaye alifanya mambo mengi ya ajabu. Aliwaua mashujaa wawili kutoka Moabu, na siku moja wakati wa teluji, alishuka katika shimo na kuua simba.


Ee Yawe, ngao yetu ni chini ya ulinzi wako. Mufalme wetu ametoka kwako, ewe Mutakatifu wa Israeli.


Wakubwa wa Edomu wamefazaishwa; viongozi wa Moabu wamepatwa na woga mukubwa; wakaaji wote wa Kanana wamevunjika moyo.


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Angalia! Ni kipoyi cha Solomono, akibebwa juu ya kiti chake cha kifalme, akizungukwa na walinzi makumi sita, mashujaa bora wa Israeli.


Kwa hiyo mikono ya kila mutu itaregea, kila mutu atavunjika moyo.


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


Umenolewa kusudi ufanye mauaji, umeangarishwa umetemete kama umeme!


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.


Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”


Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις