1 Zaidi ya hayo, Ahitofeli alimwambia Abusaloma: “Uniruhusu nichague watu elfu kumi na mbili, niondoke na kumufuatia Daudi leo usiku.
Siku hizo, shauri lolote Ahitofeli alilotoa lilikuwa kama limetolewa na Mungu. Na shauri la Ahitofeli liliheshimiwa na Daudi na Abusaloma.
Nitamushambulia akiwa amechoka na amevunjika moyo, nami nitamutia hofu kubwa. Watu wote wanaokuwa pamoja naye watakimbia. Nitamwua mufalme peke yake,
Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo, kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi.
Maana wao wako mbio kutenda maovu, haraka zao zote ni za kumwanga damu.
Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu; hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.