14 Kisha mufalme pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye, wakafika kwenye muto wakiwa wamechoka. Basi wakapumzika.
Kwa hiyo, mufalme Daudi na watu wake wakaendelea na safari, naye Simei akiwa anamufuata akimutupia mawe na kurusha mavumbi juu ya mufalme Daudi. Simei alikuwa akitembea kwenye kilele cha mulima, akielekea mufalme Daudi.
Wakati ule, Abusaloma na watu wote wa Israeli wakaenda Yerusalema na Ahitofeli akiwa pamoja nao.
Wakati Daudi alipofika kule Bahurimu, kulitokea mutu mumoja wa ukoo wa Saulo, jina lake Simei mwana wa Gera, akaanza kumulaani Daudi kwa mufululizo.
Nitamushambulia akiwa amechoka na amevunjika moyo, nami nitamutia hofu kubwa. Watu wote wanaokuwa pamoja naye watakimbia. Nitamwua mufalme peke yake,