Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 16:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Labda Yawe ataangalia mateso yangu, naye atanilipa wema kwa laana hii ninayopata leo.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 16:12
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa hiyo, mufalme Daudi na watu wake wakaendelea na safari, naye Simei akiwa anamufuata akimutupia mawe na kurusha mavumbi juu ya mufalme Daudi. Simei alikuwa akitembea kwenye kilele cha mulima, akielekea mufalme Daudi.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”


Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida; nawe uko tayari kuwasaidia siku zote. Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu, wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.


Uwaache walaani, lakini wewe unibariki; wanaonishambulia wafezeheke, nami mutumishi wako nifurahi.


Wimbo wa safari za kidini. Ee Yawe, umukumbuke Daudi, kumbuka taabu zote alizopata.


Uangalie mateso yangu na taabu yangu; unisamehe zambi zangu zote.


Hivyo utamufezehesha, kama vile kumwanga makaa ya moto juu ya kichwa chake. Yawe atakupa zawadi.


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Mungu hakuwaazibu Waisraeli vikali kama alivyowaazibu waadui zao; Waisraeli waliouawa ni wachache kuliko wale waliokuwa wanawaua.


Labda Yawe, Mungu wenu, atabadilisha nia na kuwapa baraka ya mazao, mutaweza kumutolea sadaka za chakula na kinywaji.


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


kwa sababu walikataa kuwapatia chakula na maji mulipokuwa katika njia kutoka Misri, na kwa sababu walimulipa Balamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia, awalaani.


Lakini Yawe, Mungu wenu, hakumusikiliza Balamu; pahali pake laana hiyo iligeuka kuwa baraka, kwa sababu Yawe, Mungu wenu, aliwapenda.


na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,


Wababa zetu wa kimwili walituadibisha kwa siku chache kufuatana na vile walivyoona kuwa vema. Lakini Mungu anatuadibisha kwa mafaa yetu kusudi tupate kushirikiana naye katika utakatifu wake.


Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις