Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 15:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Watumishi wote wa mufalme, Wakereti wote, Wapeleti wote, pamoja na Wagati mia sita waliomufuata mufalme Daudi kutoka muji wa Gati waliondoka pamoja naye wakimutangulia.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 15:18
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mufalme akaondoka pamoja na watu wake wote. Lakini akasimama kidogo walipofikia nyumba ya mwisho katika muji.


Daudi akatuma waaskari wake kwa vita katika vikundi vitatu: sehemu moja ya tatu ikiwa chini ya uongozi wa Yoabu, sehemu ingine ya tatu chini ya uongozi wa Abisayi mwana wa Zeruya, ndugu ya Yoabu; na sehemu ingine ya tatu chini ya uongozi wa Itayi wa muji wa Gati. Kisha mufalme Daudi akawaambia wote: “Mimi mwenyewe vilevile nitakwenda pamoja nanyi.”


Sasa Yoabu alikuwa jemadari wa waaskari wote wa Waisraeli. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa Wakereti na Wapeleti.


Abisayi akatoka akiwa pamoja na Yoabu, Wakereti na Wapeleti pamoja na mashujaa wote. Hao wote waliondoka Yerusalema kwenda kumufuata Seba mwana wa Bikiri.


Kwa hiyo, Daudi hakukuwa tayari kwa kulipeleka Sanduku la Yawe ndani ya muji wa Daudi, lakini Daudi alilipeleka katika nyumba ya Obedi-Edomu wa Gati.


Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa kiongozi wa Wakereti na Wapeleti. Wana wa Daudi wakakuwa makuhani.


Basi, kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, wote walishuka, wakamupandisha Solomono kwenye nyumbu wa mufalme Daudi, na kumupeleka mpaka Gihoni.


na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mwangalizi wa waaskari walinzi wa Daudi; wana wa Daudi walikuwa na vyeo vikubwa katika utawala wake.


Kisha, Daudi na watu wake ambao walikuwa yapata mia sita, waliondoka na kwenda popote walipoweza kwenda. Saulo aliposikia kwamba Daudi amekwisha kimbia kutoka Keila, akaiacha mipango yake yote.


Kwa hiyo Daudi akawaambia watu wake: “Kila mutu apakatie upanga wake kwenye kiuno.” Kila mutu akapakatia upanga wake, na Daudi vilevile akapakatia upanga wake. Watu yapata mia ine wakamufuata Daudi na watu mia mbili wakabaki na mizigo.


Daudi na watu wake pamoja na jamaa yake wakaishi na Akisi kule Gati. Daudi alikuwa na wake wawili: Ahinoamu kutoka Yezereheli na Abigaili mujane wa Nabali kutoka muji wa Karmeli.


Saulo aliposikia kwamba Daudi amekimbilia Gati, hakumufuata tena.


Kisha siku tatu, Daudi na watu wake wakarudi Ziklagi. Waamaleki walikuwa wamekwisha kushambulia Negebu pamoja na muji wa Ziklagi na kuuteketeza kwa moto.


Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”


Kwa hiyo, Daudi akaondoka pamoja na wale watu mia sita aliokuwa nao. Walipofika kwenye kijito cha Besori, wakawakuta wamoja kati ya watu waliotekwa wameachwa pale.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις