Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 15:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wakati Abusaloma alipokuwa akitoa sadaka, alituma ujumbe katika muji wa Gilo kwa kumwita Ahitofeli wa muji wa Gilo, aliyekuwa mushauri wa mufalme Daudi. Uasi wa Abusaloma ukazidi kupata nguvu na watu waliojiunga naye wakazidi kuongezeka.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 15:12
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakati ule, Daudi aliambiwa kwamba hata Ahitofeli alikuwa mumoja wa waasi waliojiunga na Abusaloma. Lakini Daudi akaomba akisema: “Ee Yawe, ninakuomba uyafanye mashauri ya Ahitofeli yasifanikiwe.”


Wakati ule, Abusaloma na watu wote wa Israeli wakaenda Yerusalema na Ahitofeli akiwa pamoja nao.


Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.


Ahitofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, alitandika punda wake, akaenda kwake, kwenye muji wake. Alipofika kule, alipanga vizuri mambo ya nyumba yake, akajitundika. Akakufa na kuzikwa kwenye kaburi la baba yake.


Elifeleti mwana wa Ahasibayi wa Maka; Eliamu mwana wa Ahitofeli wa Gilo;


wakatangaza sikukuu ya kufunga kula, wakakutana na kumuweka Naboti kwenye nafasi ya heshima kati ya watu.


Barua zenyewe ziliandikwa hivi: “Mutangaze kwa watu kwa kufanya sikukuu ya kufunga kula, mukutane na kumupa Naboti nafasi ya heshima kati ya watu.


Ahitofeli alikuwa mushauri wa mufalme. Ahitofeli alipokufa, alikombolewa na Yehoyada mwana wa Benaya na Abiatari. Husai Mwarki, alikuwa rafiki ya mufalme. Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi la mufalme.


Hata rafiki yangu wa moyo niliyemwamini, rafiki aliyechangia chakula nami, amegeuka kunishambulia!


Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Balamu akamwambia Balaki: Unijengee mazabahu saba hapa kisha uniletee ngombe dume saba na kondoo dume saba.


Basi, Balaki akamutwaa Balamu kwenye shamba la Sofimu, juu ya kilele cha mulima Pisiga. Hapo akajenga mazabahu saba na kutoa juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


Balaki akafanya kama vile alivyoambiwa na Balamu, kisha akatoa juu ya kila mazabahu ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja.


“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’


Wanajidai kwamba wanamujua Mungu, lakini wanamukana kwa matendo yao. Wao ni wenye machukizo, waasi hata hawafai kwa kufanya kazi yo yote nzuri.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις