17 Akamwita kijana wake aliyemutumikia, akamwambia: “Umutoshe mwanamuke huyu mbele yangu. Na ufunge mulango kwa kifungio.”
Tamari akamujibu: “Sivyo kaka yangu. Ukinifukuza utafanya ubaya mukubwa zaidi kuliko ule ulionitendea.” Lakini Amunoni hakutaka kumusikiliza.
Amunoni na yule kijana wakamutosha inje na kufunga mulango kwa kifungio. Tamari alikuwa amevaa kanzu ndefu yenye mikono mirefu maana hivi ndivyo mabikira wa mufalme walivyovaa zamani.