Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ilipokuwa kwa mwanzo wa mwaka mupya, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Daudi alimutuma Yoabu na wakubwa wake pamoja na waaskari wote wa Israeli kupigana. Nao waliteka Waamoni na kushambulia muji wa Raba. Lakini Daudi alibaki Yerusalema.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 11:1
15 Σταυροειδείς Αναφορές  

Waamoni walipoona kwamba Waaramu wamekimbia, nao vilevile walimukimbia Abisayi na kuingia katika muji. Yoabu akaacha kupigana na Waamoni, akarudi Yerusalema.


Kisha, yule nabii akamwendea mufalme wa Israeli, akamwambia: “Uongeze nguvu yako, ufikiri vizuri la kufanya. Mwaka kesho, mufalme wa Aramu atakuja kukushambulia tena.”


Halafu kwa mwaka uliofuata, mufalme Beni-Hadadi akawakusanya watu wake, akaenda katika muji wa Afeki kwa kupigana na watu wa Israeli.


Ilipokuwa wakati wa kipwa, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Yoabu akaongoza jeshi na kuharibu inchi ya Waamoni, akaenda vilevile na kuzunguka muji wa Raba kwa vita. Lakini Daudi alibaki kule Yerusalema. Naye Yoabu akashambulia muji wa Raba na kuuteka.


Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema.


Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu; Efuraimu ni kofia yangu ya chuma, na Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.


wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitavumisha sauti ya vita juu ya Raba muji wa Waamoni. –Ni ujumbe wa Yawe.– Raba utakuwa lundo la uharibifu, vijiji vyake vitateketezwa kwa moto. Halafu Israeli atatwaa tena urizi wake. Ni Yawe anayesema hivyo.


Muomboleze, enyi watu wa Hesiboni, maana muji Ai umeharibika! Mulie, enyi wabinti wa Raba! Muvae magunia, muomboleze na kukimbia huko na huko ndani ya ukuta wenu! Maana mungu Milkomu atapelekwa katika uhamisho, pamoja na makuhani wake na watumishi wake.


Kwa hiyo wamevunjika moyo na wengi wanaanguka. Nimeiweka chongo ya upanga katika milango yao yote. Umefanywa uangae kama umeme, umengarishwa kwa ajili ya mauaji.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)


Waaskari wa Wafilistini walikwenda kupigana na Waisraeli, lakini kila mara walipopigana vita, Daudi alipata ushindi kuliko watumishi wa Saulo. Hivyo jina la Daudi likazidi kusifiwa sana.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις