Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




2 Samweli 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




2 Samweli 1:16
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa hiyo, nilikwenda karibu naye na kumwua, kwa sababu nilikuwa na uhakika kwamba akianguka chini, hataweza kuishi zaidi. Lakini taji iliyokuwa juu ya kichwa chake na kikomo kilichokuwa kwenye mukono wake, vyote nimekuletea wewe, bwana wangu.”


Yawe amekulipiza kisasi kutokana na kumwanga damu ya watu wote wa jamaa ya Saulo, ambaye sasa wewe umenyanganya ufalme kwa pahali pake. Sasa, Yawe amemupa mwana wako Abusaloma ufalme. Maangamizi yamekupata kwa sababu wewe ni mwuaji.”


Maana siku utakapotoka na kuvuka kijito Kidroni, ninakuambia kweli utakufa na kubeba lazima ya kifo chako wewe mwenyewe.”


Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi; masemi yako yanashuhudia juu yako.


ikiwa umejifunga kwa maneno yako mwenyewe, utajinasa kwa ahadi uliyofanya;


Maana aliisikia sauti ya baragumu, akazarau onyo; basi lawama itakuwa juu yake mwenyewe. Lakini kama angejali hilo onyo, angeyaokoa maisha yake.


Kama mwanamuke anakaribia nyama na kulala naye, mwanamuke huyo anapaswa kuuawa na nyama huyo vilevile na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Mwanaume au mwanamuke yeyote anayekuwa mulozi au muchawi, anapaswa kuuawa kwa kupigwa mawe. Damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Mutu yeyote anayemulaani baba yake au mama yake, anapaswa kuuawa. Amemulaani baba au mama yake, kwa hiyo damu yao itakuwa juu yake mwenyewe.


Nao watu wote wakajibu: “Lazima ya damu ya mutu huyu ikuwe juu ya kichwa chetu na juu ya kichwa cha watoto wetu!”


Yule bwana akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya! Nitakuhukumu kufuatana na maneno yako. Ulijua kama mimi ni mutu mugumu, ninayetafutia nafasi nisipowekea na kuvuna nafasi nisipopanda.


Lakini wakati Wayuda walipingana naye na kumutukana, kwa hiyo akakunguta mavumbi yaliyorukia juu ya nguo zake na kuwaambia: “Lazima ya kuazibiwa kwenu ikuwe juu ya kichwa chenu wenyewe! Mimi sina kosa. Tangu sasa nitawaendea watu wa mataifa mengine.”


Ndiyo maana ninahakikisha mbele yenu leo kwamba mimi sitabeba lazima ya damu ya hata mumoja wenu atakayepotea.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


kusudi mutu asiyekuwa na kosa asiuawe katika inchi yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapatia kuwa yenu, na hivyo kuwasababisha kuwa na kosa la mauaji.


Lakini mutu yeyote akitoka inje ya nyumba yako na kwenda katika njia atabeba lazima ya kifo chake yeye mwenyewe. Lakini kama mutu yeyote atakayekuwa ndani ya nyumba yako akiguswa tu, basi lazima ya kifo chake itakuwa juu yetu.


Ndivyo watu wa Sekemu pamoja na ndugu yao Abimeleki walivyoazibiwa kwa sababu waliwatendea kwa ukali wana makumi saba wa Yerubali. Azabu ya mauaji hayo iliwapata maana Abimeleki aliwaua akisaidiwa na hao watu wa Sekemu.


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


Lakini Daudi akamwambia Abisai: “Usimwangamize; maana nani anaweza kunyoosha mukono wake juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe, naye asiazibiwe?


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις