Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Yoane 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Yoane 1:3
38 Σταυροειδείς Αναφορές  

Sikia! Hayo yote nimeyaona kwa macho yangu. Nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Uniokoe toka kinywa cha simba; uokoe nafsi yangu zaifu toka pembe za mbogo hao.


Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.


Tena ukienda nasi chochote chema Yawe atakachotutendea, ndicho utakachotendewa nawe vilevile.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Mutu aliyeona mambo hayo ndiye anayeyashuhudia, nao ushuhuda wake ni wa kweli. Na anajua kama anasema ukweli, kusudi mupate kuamini vilevile.


Na sasa sisi tunahubiri Habari Njema kwenu kwamba, ile Mungu aliyoitoa kwa babu zetu


‘Muangalie, ninyi wenye kuzarau, mupigwe na mushangao na mutoweke! Maana katika siku hizi nitafanya jambo ambalo ninyi musingeweza kusadikia hata wangewaelezea.’ ”


Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.


Ni vile kwa sababu niliwatangazia mupango wote wa Mungu pasipo kuwaficha kitu.


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


Ndiyo wamefanya vile kwa mapenzi yao, lakini vilevile ilikuwa mapaswa kwao kuwasaidia. Kwa maana ikiwa watu wa mataifa wameshirikiana baraka za kiroho na Wayuda, imewapasa watu wa mataifa mengine kuwasaidia Wayuda katika mahitaji ya kimwili.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Mungu ni mwaminifu katika ahadi zake, yeye aliyewaita ninyi muishi katika ushirika pamoja na Mwana wake Yesu Kristo, Bwana wetu.


Wandugu zangu, sasa ninataka kuwakumbusha Habari Njema niliyowatangazia, ile muliyopokea na kuishika imara.


Nao mupango ule ni kwamba kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapewa sehemu yao ya urizi kutoka kwa Mungu pamoja na Wayuda. Watu wale ni viungo vya mwili mumoja, nao wanapokea vilevile sehemu ya vitu Mungu alivyoahidi kwa njia ya Yesu Kristo.


Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.


Maisha yenu katika kuungana kwenu na Kristo si yanawatia ninyi nguvu? Nao upendo wake si unawafariji ninyi? Si munaishi katika ushirika na Roho Mutakatifu? Si muko na moyo mwema na wa huruma?


Kitu ninachotaka tu, ni kumujua Kristo na uwezo wa ufufuko wake na kushirikiana naye katika mateso yake, nako kufa kwangu kufanane na kufa kwake.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Na wale wanaokuwa na wabwana waamini, wasiwakosee heshima kwa sababu wao ni wandugu. Wanapaswa kuwatumikia vizuri zaidi, kwa maana wao ni wandugu waamini na wapendwa, nao wanashiriki faida ya kazi yao. Hayo ndiyo maneno unayopaswa kufundisha na kuhubiri.


Kwa maana anasema: “Ee Mungu, nitatangaza jina lako kwa wandugu zangu, nitakusifu katikati ya mukutano.”


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.


Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.


Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις