Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Wakorinto 2:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nasi tunaposema hatutumii maneno yanayotokana na hekima ya kimutu, lakini maneno yanayotokana na Roho wa Mungu, tukieleza maneno ya kiroho kwa watu wanaokuwa wa Roho.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Wakorinto 2:13
14 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mafundisho yangu na mahubiri yangu hayakutolewa kwa maneno ya werevu na hekima ya kimutu, lakini katika onyesho la uwezo wa Roho wa Mungu,


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Kristo hakunituma kwa kubatiza, lakini amenituma kwa kutangaza Habari Njema. Amenituma kuitangaza bila kutumia hekima ya usemi, kusudi uwezo unaotokana na kufa kwa Kristo juu ya musalaba usihesabiwe kuwa bure.


Wandugu zangu, wakati nilipokuja kwenu kuwapasha habari ya siri ya Mungu, sikutumia maneno magumu wala hekima ya dunia.


Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.


Munapoongea, museme maneno ya zaburi, mumusifu Bwana na kumwabudu kwa nyimbo za kiroho. Mumwimbie na kumushangilia kwa moyo wenu wote.


Mutu anayesema kwa luga ya ajabu hasemi na watu lakini anasema na Mungu, kwa maana hakuna mutu anayemusikia. Kwa uwezo wa Roho, mutu yule anasema mafumbo.


Ikiwa tumepanda mbegu ya kiroho ndani yenu, basi kuna jambo gani kubwa kama nasi tukitazamia kupata vifaa vya kimwili toka kwenu?


kwa sababu Roho Mutakatifu atawafundisha saa ile ile maneno munayopaswa kusema.”


Wote wakapewa Roho Mutakatifu na kuanza kusema kwa luga mbalimbali kwa kadiri Roho alivyowawezesha kusema.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις