Basi mufalme, watumishi wake na wakaaji wote wa Misri wakaamuka usiku. Kukakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri kwa maana hakukuwa hata nyumba moja ambamo mutu hakukufa.
Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.
Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba, halafu anakutana na dubu! Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake, na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka.
“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”