Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 5:10
13 Σταυροειδείς Αναφορές  

Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.


Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”


Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi, pamoja na mutawala wa Asikeloni. Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni, na Wafilistini wote waliobaki wataangamia. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Muende Kalne, muangalie. Tokea kule muende mpaka katika ule muji mukubwa wa Hamati, kisha mutelemuke mpaka Gati kwa Wafilistini. Mutatambua kwamba ninyi si bora kuliko falme zile, hata kama eneo lao ni ndogo zaidi ya lenu.


ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,


Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekuroni, ukazunguka kuelekea Sikeroni ambapo ulipita karibu na mulima Bala mpaka Yabuneli ukaishia katika bahari ya Mediteranea.


Watu wa kabila la Yuda vilevile waliteka miji ya Gaza na eneo lake, Askeloni na eneo lake, na Ekuroni na eneo lake.


Halafu watu wa Israeli na watu wa Yuda walianza kupiga kelele za ushindi, wakawafuatilia Wafilistini mpaka Gati, kwenye milango ya muji wa Ekroni, hata Wafilistini walioumizwa katika vita walikufa katika njia tangu Saraimu mpaka Gati na Ekroni.


Kisha wakatuma ujumbe na kukusanya wakubwa wa Wafilistini na kuwaambia: “Mulirudishe Sanduku la Mungu wa Israeli kwa nafasi yake, kusudi lisituue sisi pamoja na watu wetu.” Walifanya hivyo kwa sababu kulikuwa hofu kubwa katika muji muzima kwa sababu Mungu alikuwa anawaazibu vikali.


Lakini kisha kulipeleka kule Gati, Yawe akauazibu muji huo, akitia hofu kubwa katika muji, na akawapiga wanaume wa muji huo, vijana kama vile wazee, kwa kuwaletea majipu.


Nyuma ya Sanduku la Yawe kukaa katika inchi ya Wafilistini kwa muda wa miezi saba,


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις