Yule kijana akamujibu: “Kwa bahati, nilikuwa juu ya mulima Gilboa. Nilimwona Saulo akiegemea mukuki wake na magari ya waaskari wapanda-farasi ya waadui zake yalikuwa yanamusonga sana.
Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.
Saulo na mwana wake Yonatani pamoja na watu waliokuwa pamoja nao, walikaa kule Gibea katika inchi ya Benjamina na Wafilistini walipiga kambi kule Mikimasi.
Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.
Hata Waisraeli wengine waliokuwa wamejificha kwenye inchi ya milima ya Efuraimu, waliposikia kwamba Wafilistini walikuwa wanakimbia, nao vilevile wakawafuatilia na kuwapiga.
Yonatani akamwambia: “Usiogope, baba yangu Saulo hatakupata. Wewe utakuwa mufalme wa Israeli, mimi nitakuwa wa pili wako. Hata Saulo baba yangu anajua jambo hili.”
Zaidi ya hayo, Yawe atakutia wewe pamoja na Waisraeli wote katika mikono ya Wafilistini. Kesho, wewe na wana wako mutakuwa pamoja nami. Hata waaskari wa Israeli, Yawe atawatia katika mikono ya Wafilistini.”