Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 30:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha siku tatu, Daudi na watu wake wakarudi Ziklagi. Waamaleki walikuwa wamekwisha kushambulia Negebu pamoja na muji wa Ziklagi na kuuteketeza kwa moto.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 30:1
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakati ule, Isaka alikuwa ameondoka Beri-Lahai-Roi, akakaa pande za Negebu.


Nyuma ya kufa kwa Saulo, Daudi alirudi kisha kuwashinda Waamaleki, akakaa Ziklagi kwa muda wa siku mbili.


Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.


yeye aliniuliza mimi ni nani, nami nikamwambia kwamba mimi ni Mwamaleki.


Watumishi wote wa mufalme, Wakereti wote, Wapeleti wote, pamoja na Wagati mia sita waliomufuata mufalme Daudi kutoka muji wa Gati waliondoka pamoja naye wakimutangulia.


Basi, Daudi alipokuwa Ziklagi, watu hawa wa kabila la Manase wakamwendea: Adina, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Siletayi. Kila mumoja wao alikuwa kiongozi wa kundi la watu elfu moja katika kabila la Manase.


Wakamusaidia Daudi kupigana na makundi ya washambulizi, maana wote walikuwa waaskari mashujaa na majemadari wa waaskari.


waliwakusanya watu wao wote, wakaenda kupigana na Isimaeli. Walimukuta kwenye kisima kikubwa cha Gibeoni.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”


Saulo aliwashinda Waamaleki kuanzia Havila mpaka Suri, kwa upande wa mashariki wa Misri.


Alimukamata mateka mufalme Agagi wa Waamaleki akiwa angali muzima. Akawaua watu kwa makali ya upanga.


Siku hiyo, Akisi akamupa muji wa Ziklagi. Kwa hiyo, tangu siku hiyo muji wa Ziklagi ukakuwa mali ya wafalme wa Yuda.


Sasa, wewe pamoja na watumishi wa bwana wako Saulo waliokuja pamoja nawe, kesho asubui mapema, muamuke na kuondoka mara tu kunapopambazuka.”


Kwa hiyo, kesho yake asubui, Daudi pamoja na watu wake waliondoka kurudi katika inchi ya Wafilistini. Lakini hao Wafilistini wakaenda Yezereheli.


Lakini wakubwa wa Wafilistini walimukasirikia sana Akisi, wakamwambia: “Umurudishe aende pahali ulipomupa akae. Asiende hata kidogo pamoja nasi kwa vita, kama sivyo wakati wa vita atageuka na kuwa adui yetu. Hauoni kwamba mutu huyu atapata njia nzuri ya kupatana na bwana wake halafu kuwa adui yetu katika vita?


Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις