Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 29:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wafilistini walikusanya makundi yao yote ya waaskari kule Afeki, na Waisraeli walipiga kambi kwenye chemichemi ya bonde la Yezereheli.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 29:1
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kule, Abeneri akamusimika Isiboseti kuwa mufalme wa inchi ya Gileadi, Asheri, Yezereheli, Efuraimu na Benjamina na Israeli yote.


Wafilistini waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mufalme wa Waisraeli, wote walitoka kwenda kumutafuta, lakini yeye alipata habari, akaingia ndani ya makimbilio.


Waliobaki, walikimbilia katika muji wa Afeki. Kule, kuta za muji ziliwaangukia na kuwaua watu elfu makumi mbili na saba waliobakia. Beni-Hadadi vilevile alikimbia na kujificha katika chumba fulani cha ndani, katika muji.


Nyuma ya mambo hayo, Naboti wa muji wa Yezereheli alikuwa na shamba lake la mizabibu kule Yezereheli, karibu na nyumba ya Ahabu, mufalme wa Samaria.


Tena, Yawe anasema hivi juu ya Yezebeli: ‘Imbwa wataukula mwili wa Yezebeli humuhumu katika muji wa Yezereheli.


Yehu alipofika Yezereheli, Yezebeli alikuwa amekwisha kupata habari ya mambo yaliyotokea. Alijipakaa rangi kwenye macho na kuchanua nywele zake, kisha akaenda kwenye dirisha na kuangalia chini.


Kisha walirudi na kumupasha Yehu habari hii, naye akasema: “Hivi ndivyo Yawe alivyotabiri kwa njia ya mutumishi wake Elia wa muji wa Tisibe akisema: ‘Imbwa wataukula mwili wa Yezebeli katika shamba la Yezereheli.


Waedomu na Waisimaeli, Wamoabu na Wahagari;


mufalme wa Afeki, mufalme wa Lasaroni,


Nao wakamujibu: “Ni kweli kwamba inchi hii ya milima haitutoshi. Hata hivyo wale Wakanana wote wanaokaa kwenye bonde wana magari ya chuma, vilevile wale wote wanaokaa Beti-Seani pamoja na vijiji vyake, na wale wanaoishi katika Bonde la Yezereheli.”


Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya: Yezereheli, Kesuloti, Sunemu, Hafaraimu, Sioni, Anaharati, Rabiti, Kisioni, Ebesi, Remeti, Eni-Ganimu, Eni-Hada na Beti-Pasesi. Vilevile, mupaka wao ulifika Tabori, Sahasuma, Beti-Semesi na kuishia kwenye muto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.


Uma, Afeki na Rehobu. Jumla ya miji waliyopewa ni makumi mbili na mbili pamoja na vijiji vyake.


Wamidiani, Waamaleki na watu wote wanaokaa pembeni ya muto Yordani wakapiga kambi zao katika bonde la Yezereheli.


Yerubali, ni kusema Gideoni na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaamuka mapema, wakapiga kambi yao katika bonde karibu na chemichemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa upande wao wa kaskazini katika bonde karibu na mulima More.


Akamupa Saulo, akawapa vilevile watumishi wake, nao wakakula. Halafu wakaondoka na kwenda zao wakati uleule wa usiku.


Wafilistini walikusanyika na kupiga kambi yao kule Sunemi; na Saulo aliwakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao kwenye mulima Gilboa.


Wakati huo, Wafilistini walikutana pamoja, wapigane na Waisraeli. Waisraeli walipiga kambi yao kule Ebeni-Ezeri, na Wafilistini wakapiga kambi yao kule Afeki.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις