Halafu yule mwanamuke alimwendea Saulo, na alipoona kwamba Saulo ameshikwa na hofu sana, alimwambia: “Mimi mutumishi wako nimehatarisha maisha yangu kwa kufanya kile ulichoniambia nikufanyie.
Lakini Saulo alikataa na kusema: “Sitakula.” Lakini watumishi pamoja na yule mwanamuke, walimusihi akule, naye akawasikiliza. Kwa hiyo alisimama kutoka chini na kuikaa kwenye kitanda.