Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 27:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 27:8
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa hiyo, Yoabu aliondoka, akaenda Gesuri kumuleta Abusaloma katika Yerusalema.


Abusaloma akamujibu: “Nilikutumia ujumbe, ukuje huku kusudi nikutume kwa mufalme, umwulize: ‘Kwa nini niliondoka Gesuri? Ingekuwa bora kwangu kubaki kule.’ Sasa unisaidie nipate kumwona mufalme. Kama nina kosa basi, aniue!”


Maana, mimi mutumishi wako, nilipoishi kule Gesuri katika inchi ya Aramu, nilimufanyia Yawe kiapo nikisema kama Yawe akinirudisha Yerusalema basi, nitamwabudu yeye.”


Kisha, Yoabu pamoja na watu wa Daudi walirudi kutoka kwenye mashambulio, wakaleta vitu vingi. Lakini Abeneri hakukuwa pamoja na Daudi kule Hebroni maana Daudi alikuwa amemwaga aende zake, naye akaondoka kwa amani.


Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli; Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;


ni kusema Aramu, Moabu, Amoni, Filistini, Amaleki. Aliteka vilevile vitu vya mufalme Hadadezeri mwana wa Rehobu mufalme wa Zoba.


Lakini falme za Gesuri na Aramu ziliwashambulia na kuwanyanganya miji ya Yairi, Kenati pamoja na vijiji vyake, jumla ya miji ilikuwa makumi sita. Hao wote walikuwa wazao wa Makiri, baba ya Gileadi.


Kisha, Musa akawaongoza Waisraeli kutoka bahari Nyekundu, wakaenda mpaka kwenye jangwa la Suri. Wakasafiri kwa muda wa siku tatu katika jangwa bila kuona maji yoyote.


Waamaleki walikuja na kupigana na Waisraeli kule Refidimu.


Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.


Halafu Waamaleki na Wakanana, waliokuwa wakiishi katika inchi hiyo ya milima, wakashuka, wakawashambulia na kuwashinda. Wakawafukuza mpaka muji wa Horma.


Utawala wake ulienea mpaka kule kwenye mulima Hermoni, kule Saleka, Basani yote mpaka kwa mipaka ya Wagesuri na Wamakati, nusu ya Gileadi hata kwa mupaka wa inchi ya mufalme Sihoni wa Hesiboni.


Hata hivyo, Wagesuri na Wamakati hawakufukuzwa lakini wanaishi kati ya Waisraeli mpaka leo.


Sehemu hizo ni: inchi yote ya Wafilistini na inchi yote ya Wagesuri,


Waefuraimu hawakuwafukuza Wakanana walioishi Gezeri. Wakanana hao waliendelea kukaa kati ya watu wa Efuraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.


Watu wa kabila la Efuraimu hawakuwafukuza Wakanana walioishi kule Gezeri, na hawa waliishi kule pamoja na watu wa Efuraimu.


Akisi akamwita Daudi na kumwambia: “Kama vile Yawe anavyoishi, umekuwa mutu wa usawa. Ingekuwa jambo zuri kwangu tuende wote katika vita, kwa maana sijaona jambo baya lolote kwako tangu siku ile ulipokuja kwangu mpaka leo hii. Hata hivyo, wakubwa hawajapendezwa nawe.


Kisha siku tatu, Daudi na watu wake wakarudi Ziklagi. Waamaleki walikuwa wamekwisha kushambulia Negebu pamoja na muji wa Ziklagi na kuuteketeza kwa moto.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις