Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.
Wakubwa wa waaskari wa Wafilistini waliuliza: “Waebrania hawa wanafanya nini hapa?” Akisi akawajibu wale wakubwa wa Wafilistini: “Huyu ni Daudi, mutumishi wa Saulo mufalme wa Israeli; naye amekuwa nami kwa miaka fulani. Na tangu alipokimbilia kwangu, sijamupata na kosa lolote.”