Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 26:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Lakini Yawe anakataza nisinyooshe mukono wangu juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe. Lakini twaa mukuki wake unaokuwa karibu na kichwa chake pamoja na mufuko wake wenye maji, halafu tujiendee zetu.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 26:11
11 Σταυροειδείς Αναφορές  

Daudi akamwuliza: “Ilikuwa namna gani wewe haukuogopa kuunyoosha mukono wako na kumwua muchaguliwa wa Yawe?”


Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”


Halafu Abisayi mwana wa Zeruya akasema: “Si Simei anapaswa kuuawa maana alimulaani muchaguliwa wa Yawe?”


Juu ya matendo watu wanayotenda, mimi nimetii amri yako, sikushika njia za watesaji wakali.


Musimurudishie mutu ubaya kwa ubaya. Mukuwe na roho ya kufanya mema mbele ya watu wote.


Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.”


Angalia, baba yangu, angalia pindo hili la nguo yako katika mikono yangu. Kwa kulikata pindo la nguo yako bila kukuua, unaweza sasa kujua kwa hakika kwamba mimi si mwovu wala mwasi. Mimi sijatenda zambi juu yako ingawa wewe unaniwinda uniue.


Saulo alipokuwa anasafiri, alifika kwenye pango moja lililokuwa karibu na zizi la kondoo, akaingia mule ndani ya pango kwa kujisaidia. Daudi na watu wake walikuwa wakiikaa ndani kabisa ya pango lile.


Daudi akaanza kufazaika ndani ya moyo kwa sababu alikata pindo la nguo ya Saulo kwa siri.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις