Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 25:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kwa hiyo Daudi akawaambia watu wake: “Kila mutu apakatie upanga wake kwenye kiuno.” Kila mutu akapakatia upanga wake, na Daudi vilevile akapakatia upanga wake. Watu yapata mia ine wakamufuata Daudi na watu mia mbili wakabaki na mizigo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 25:13
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Watumishi wote wa mufalme, Wakereti wote, Wapeleti wote, pamoja na Wagati mia sita waliomufuata mufalme Daudi kutoka muji wa Gati waliondoka pamoja naye wakimutangulia.


Mutu asiyekuwa mwepesi wa hasira ana akili nyingi, lakini anayekasirika upesi anaongeza upumbafu.


Asiyekuwa mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwenye nguvu. Anayetawala nafsi yake ni bora kuliko anayetaka muji.


Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.


Haifai mutu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka anajikwaa.


Usiseme: “Nitalipiza ubaya niliotendewa.” Umutegemee Yawe naye atakusaidia.


Mambo uliyoona kwa macho yako, usiharakishe kuyapeleka katika tribinali; maana utafanya nini kwa mwisho, kama jirani yako anakupatisha haya?


Hivyo, Waisraeli wakatwaa vyakula vyao, bila kumwuliza Yawe shauri.


Watu wote waliogandamizwa au waliokuwa na madeni au wale wenye huzuni walijiunga na Daudi. Jumla yao ilikuwa watu yapata mia ine, naye akakuwa kiongozi wao.


Kisha, Daudi na watu wake ambao walikuwa yapata mia sita, waliondoka na kwenda popote walipoweza kwenda. Saulo aliposikia kwamba Daudi amekwisha kimbia kutoka Keila, akaiacha mipango yake yote.


Basi, wale vijana wa Daudi walirudi na kumwambia Daudi namna walivyojibiwa.


Kwa hiyo, mara moja Daudi na watu wake mia sita wakaenda kwa Akisi mwana wa Maoki, mufalme wa Gati.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις