Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 25:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kisha Nabali akawajibu watumishi wa Daudi: “Daudi ni nani? Mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumishi wengi wanaowakimbia wabwana zao.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 25:10
14 Σταυροειδείς Αναφορές  

Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali, walimwambia: “Hatuna ushirika wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Murudie kwenu, enyi watu wa Israeli! Uitunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi kila mutu kwake.


Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”


Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.


Usiulize: “Kwa nini nyakati za zamani zilikuwa bora kuliko za sasa?” Hauulizi hivyo kwa kutumia hekima.


Wapumbafu hawataitwa tena wenye cheo, wala watu wa ovyoovyo hawataitwa tena waheshimiwa.


Matendo ya watu wadanganyifu ni mabaya; hao wanatunga maneno mabaya kwa kumwangamiza masikini kwa maneno ya uongo, hata kama masikini ni mwenye sheria.


Gali mwana wa Ebedi, akasema: “Abimeleki ni nani? Sisi hapa Sekemu ni watu wa aina gani hata tumutumikie Abimeleki? Gideoni na Zebuli jemadari wake walimutumikia Hamori baba wa Sekemu, lakini kwa nini basi, sisi tumutumikie Abimeleki?


Kwa hiyo Saulo akawaka hasira juu ya Yonatani, akamwambia: “Mwana wa imbwa wewe! Ninajua kwamba umejichagulia mwana wa Yese kwa ajili ya haya yako mwenyewe, na kumufezehesha mama yako!


Watu wote waliogandamizwa au waliokuwa na madeni au wale wenye huzuni walijiunga na Daudi. Jumla yao ilikuwa watu yapata mia ine, naye akakuwa kiongozi wao.


Wale vijana wa Daudi walikwenda na kumwambia Nabali kama walivyoagizwa na Daudi. Halafu wakangojea kidogo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις