Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 23:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Basi, Daudi akamwomba Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini hawa?” Yawe akamujibu: “Ndiyo, kwenda kuwashambulia Wafilistini na kuuokoa muji wa Keila.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 23:2
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”


Basi, Daudi alimwuliza Yawe shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia Daudi: “Kwenda, maana hakika nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”


Daudi alipomwomba Yawe shauri, Yawe alimwambia: “Usiwashambulie kutoka hapa unapokuwa, lakini zunguka nyuma yao na kuwashambulia kutokea mbele ya miti ya miforosadi.


Halafu Daudi akamwomba Mungu shauri: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono yangu?” Naye Yawe akamwambia: “Kwenda, nitawatia katika mikono yako.”


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


Ninajua, ee Yawe, mwanadamu hana uwezo juu ya maisha yake; hakuna mutu anayeweza kuongoza maisha yake.


Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.


Hivyo, Waisraeli wakatwaa vyakula vyao, bila kumwuliza Yawe shauri.


Nyuma ya kifo cha Yoshua, Waisraeli walimwuliza Yawe: “Ni kabila gani litakwenda kupigana kwanza na Wakanana?”


Wakamwuliza Mungu tena: “Kuna mutu zaidi anayekuja?” Yawe akawajibu: “Anajificha kwenye mizigo.”


Hivyo, Saulo akamwuliza Mungu: “Niende kuwashambulia Wafilistini? Utawatia katika mikono ya Waisraeli?” Lakini Mungu hakujibu kitu siku hiyo.


Lakini watu wa Daudi wakamwambia: “Kama tukiwa hapahapa katikati ya inchi ya Yuda tunaogopa, itakuwa namna gani basi tukienda Keila na kushambulia waaskari wa Wafilistini?”


Daudi akamwomba tena Yawe shauri, naye Yawe akamwambia: “Simama uende Keila maana nitawatia Wafilistini katika mikono yako.”


Abiatari mwana wa Ahimeleki, alipokimbilia kwa Daudi kule Keila, alikwenda na kizibao cha kuhani.


Daudi akamwomba Yawe shauri: “Nikifuata kundi hili nitalikamata?” Yawe akamujibu: “Ulifuate maana utalipata na kuwaokoa hao waliotekwa.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις