Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 23:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yonatani akamwambia: “Usiogope, baba yangu Saulo hatakupata. Wewe utakuwa mufalme wa Israeli, mimi nitakuwa wa pili wako. Hata Saulo baba yangu anajua jambo hili.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 23:17
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe yuko nami, siogopi kitu; mwanadamu ataweza kunifanya nini?


Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.


Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.


Muimarishe mikono zaifu, mukaze magoti yanayoregea.


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Tulipofika Roma, Paulo akapewa ruhusa ya kujilipia nyumba ya kupanga ambamo atakaa pamoja na askari mumoja mwenye kumuchunga.


Lakini ikiwa vimeanzishwa na Mungu, hamutaweza kuwazuiza. Basi mujiangalie vizuri musikuje kuonekana kuwa munapigana na Mungu!”


kwa hiyo nitawafikia nitakapokwenda Spania. Ninatumaini kupitia kule na kuonana nanyi, na kisha kufurahi kwanza pamoja nanyi kwa muda mufupi, ningetamani kupata musaada wenu kwa ajili ya safari ile.


Kwa sababu hii tunaweza kusema kwa uhodari: “Bwana ndiye musaidizi wangu; sitaogopa kitu. Mwanadamu ataweza kunifanya nini?”


Wewe, haujui kwamba wakati mwana wa Yese angali anaishi katika dunia, wewe hautaweza kuwa na uhakika wa kuwa mufalme wa inchi hii? Sasa hivi kwenda umulete hapa kwangu, kwa sababu anapaswa kuuawa.”


Wewe, ukae pamoja nami, wala usiogope. Maana, anayetafuta kuyaangamiza maisha yangu anatafuta hata yako vilevile. Ukiwa pamoja nami, uko salama kabisa.”


Leo, umeonyesha jinsi unavyokuwa muzuri kwangu. Haukuniua ijapokuwa Yawe alinitia katika mikono yako.


Mutu akimukamata adui yake atamwacha aende salama? Kwa lile ulilonitendea, Yawe akupe zawadi njema!


Sasa nimejua kwamba hakika utakuwa mufalme wa Israeli, na ufalme wa Israeli utaimarishwa chini yako.


Saulo alipokuwa anasafiri, alifika kwenye pango moja lililokuwa karibu na zizi la kondoo, akaingia mule ndani ya pango kwa kujisaidia. Daudi na watu wake walikuwa wakiikaa ndani kabisa ya pango lile.


Nyuma ya Yawe kukutendea mazuri yote aliyokuahidi, na kukuchagua kuwa mutawala wa Israeli,


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις