Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 20:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 20:41
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha Yakobo akamubusu Rakeli na kulia kwa sauti.


Labani aliposikia habari za mwipwa wake Yakobo, alikwenda mbio kumupokea, akamukumbatia, akamubusu, akamukaribisha ndani ya nyumba yake. Yakobo akamwelezea Labani mambo yote yaliyotokea.


Basi, Esau akakwenda mbio kumupokea Yakobo, akamukumbatia, kumubusu kwenye shingo, na wote wawili wakalia.


Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.


Wakamujibu: “Mutumishi wako, baba yetu, yuko salama na angali muzima.” Kisha wakainama kwa heshima.


Akiwa angali analia, Yosefu akawakumbatia wandugu zake na kuwabusu. Hapo ndipo wandugu zake walipoweza kuzungumuza naye.


Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.


Ninasikitika kwa ajili yako, ndugu yangu Yonatani. Umekuwa kwangu mutu wa kupendeza siku zote. Pendo lako kwangu limekuwa la ajabu, la ajabu kuliko la mwanamuke.


Huyo mwanamuke kutoka Tekoa akaenda kwa mufalme, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme, akamwambia: “Ee mufalme, unisaidie.”


Mufalme akamwambia: “Kimuhamu atakwenda nami, na nitamutendea lolote unaloona ni zuri. Na lolote utakalotaka nikutendee, nitakutendea.”


Basi, Mefiboseti mwana wa Yonatani na mujukuu wa Saulo akaenda kwa mufalme Daudi, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme Daudi. Daudi akamwita: “Mefiboseti!” Naye akamujibu: “Ndiyo! Mimi mutumishi wako niko hapa.”


Batiseba aliinama kwa heshima mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: “Unataka nini?”


Nao watu wakamwambia mufalme: “Nabii Natani yuko hapa.” Naye alipomufikia mufalme, aliinama mbele ya mufalme mpaka uso ukafika chini kwenye udongo.


Batiseba akainama uso mpaka chini, kwa heshima mbele ya mufalme, na kusema: “Bwana wangu mufalme Daudi aishi milele!”


Na wote walilia sana wakimukumbatia na kumubusu.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Kwa sababu Yonatani alimupenda Daudi kama roho yake, alifanya agano naye.


Yonatani akamupatia yule kijana silaha zake na kumwambia: “Kwenda urudi katika muji.”


Kisha, Daudi naye akasimama, akatoka ndani ya pango na kumwita Saulo: “Bwana wangu mufalme!” Mufalme Saulo alipoangalia nyuma, Daudi aliinama mpaka chini, kwa kumuheshimu Saulo.


Abigaili alipomwona tu Daudi, akashuka mara moja kutoka juu ya punda wake, na kuinama mbele ya Daudi mpaka uso wake ukagusa chini.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις