Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 19:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Alipomwua yule Mufilistini Goliati, alihatarisha maisha yake, naye Yawe aliwapa Waisraeli ushindi mukubwa. Wewe ulipoona jambo lile ulifurahi. Kwa nini unataka kutenda zambi kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa kwa kumwua Daudi bila sababu?”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 19:5
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Lakini Eleazari alisimama imara na kupigana na Wafilistini mpaka mukono wake uliposhindwa kupindika, ukabaki umebania upanga wake. Siku hiyo, Yawe alijipatia ushindi mukubwa. Nyuma ya ushindi ule, Waisraeli walirudi pahali Eleazari alipokuwa na kuteka vitu kutoka kwa Wafilistini waliouawa.


Lakini wakasimama imara katikati ya shamba lile kwa kulikinga, wakaua Wafilistini; Yawe akawaokoa kwa kuwapa ushindi mukubwa.


Wale mashujaa wake watatu wakatoka, wakapenya katikati ya kambi ya jeshi la Wafilistini, wakaenda na kuchota maji katika kisima cha Betelehemu, karibu na mulango wa muji, wakamuletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyakunywa, na kwa pahali pake akayamwanga chini kama sadaka kwa Yawe


Wananilipa mabaya kwa mazuri yangu, na chuki kwa mapendo yangu.


Maisha yangu yako katika hatari siku zote, lakini sisahau sheria yako.


Usimwache anayekutumainia kupata haya; lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.


Ninaregea kwa ajili ya kulalamika, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.


Wao wanapatana kuwaangamiza watu wa haki, na kuwahukumu watu wasiokuwa na kosa wauawe.


Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.


Lakini mujue kwa hakika kwamba mukiniua, mutakuwa mumejiletea laana ninyi wenyewe kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa, na kuleta laana juu ya muji huu na wakaaji wake. Maana, ni kweli kwamba Yawe alinituma niwaambie mambo hayo kusudi muyasikie.


Basi Pilato alipoona kwamba hataweza kufanya kitu, isipokuwa tu kuongeza fujo, akatwaa maji na kunawa mikono yake mbele ya watu wote, akisema: “Lazima ya damu ya mutu huyu isikuwe juu ya kichwa changu! Maneno haya yanawaangukia.”


Akawaambia: “Nimekosa kwa kumutoa mutu huyu asiyekuwa na kosa auawe.” Lakini wao wakamujibu: “Jambo hilo halituelekei. Ni kazi yako wewe mwenyewe!”


Lakini wamefanya hivi kusudi maneno haya yaliyoandikwa katika Sheria yao yatimie: ‘Wamenichukia pasipo sababu.’


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


kwa sababu yeye alikuwa karibu kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo. Alihatarisha maisha yake kwa kuja kuniletea musaada ule ambao ninyi wenyewe musingeweza kunipatia.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Nilipoona kwamba hamukukuja kuniokoa, nikahatarisha maisha yangu, nikavuka kwenda kupigana na Waamoni, naye Yawe akawatia katika mikono yangu. Kwa nini sasa munakuja kupigana na mimi?”


Kwa maana baba yangu alihatarisha maisha yake kwa kuwapigania na kuwakomboa kutoka kwa Wamidiani!


Lakini Saulo akawaambia: “Hakuna mutu yeyote atakayeuawa leo, kwa sababu katika siku hii, Yawe ameikomboa Israeli.”


Lakini watu wakamwambia Saulo: “Kwa nini Yonatani, aliyeletea Waisraeli ushindi huu mukubwa, auawe? Haiwezikani hata kidogo. Kama vile Yawe anavyoishi, hata unywele mumoja wa kichwa chake hautaanguka chini. Alichokifanya leo, amekifanya kwa musaada wa Yawe.” Kwa hiyo, watu walimukomboa Yonatani naye hakuuawa.


Saulo alimusikiliza Yonatani, kisha akaapa: “Kama vile Yawe anavyoishi, sitamwua Daudi.”


Yonatani akamujibu: “Kwa nini auawe? Amefanya nini?”


Ahimeleki akamujibu: “Kati ya watumishi wako, Daudi ndiye mukubwa wa kuaminika kuliko wote. Yeye ni mukwe wako wewe mufalme mwenyewe, mukubwa wa waaskari wako walinzi na anaheshimiwa kuliko wote katika nyumba yako.


Halafu yule mwanamuke alimwendea Saulo, na alipoona kwamba Saulo ameshikwa na hofu sana, alimwambia: “Mimi mutumishi wako nimehatarisha maisha yangu kwa kufanya kile ulichoniambia nikufanyie.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις