Lakini mupwa wa Paulo akapata habari ya vile watu wale wanavyovizia kumwua Paulo. Halafu akaenda katika upango wa waaskari na kumujulisha Paulo habari ile.
Mimi nitakuja na kusimama karibu na baba yangu kule katika shamba pahali utakapokuwa. Pale nitaongea naye juu yako, na kitu chochote nitakachogundua kutoka kwake, nitakuelezea.”
Yonatani akamujibu: “Jambo hilo lipite mbali nawe. Hautakufa. Baba yangu hafanyi jambo lolote, likuwe kubwa au dogo, bila kunielezea. Hata jambo hili hawezi kunificha. Sivyo inavyokuwa hata kidogo.”
Daudi akamwambia: “Kesho ni sikukuu ya mwandamo wa mwezi, nami nilipaswa kuwa kwenye meza kwa kula pamoja na mufalme. Lakini uniache, niende kujificha kule katika shamba mpaka siku ya tatu magaribi.