Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 17:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Halafu watu wa Israeli na watu wa Yuda walianza kupiga kelele za ushindi, wakawafuatilia Wafilistini mpaka Gati, kwenye milango ya muji wa Ekroni, hata Wafilistini walioumizwa katika vita walikufa katika njia tangu Saraimu mpaka Gati na Ekroni.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 17:52
10 Σταυροειδείς Αναφορές  

Lakini Eleazari alisimama imara na kupigana na Wafilistini mpaka mukono wake uliposhindwa kupindika, ukabaki umebania upanga wake. Siku hiyo, Yawe alijipatia ushindi mukubwa. Nyuma ya ushindi ule, Waisraeli walirudi pahali Eleazari alipokuwa na kuteka vitu kutoka kwa Wafilistini waliouawa.


Basi, mufalme wa Israeli akashinda vita, akateka farasi na magari ya vita mengi, na kuwaua Waaramu kwa wingi.


Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekuroni, ukazunguka kuelekea Sikeroni ambapo ulipita karibu na mulima Bala mpaka Yabuneli ukaishia katika bahari ya Mediteranea.


Waisraeli wa kabila la Nafutali, Aseri, na Manase, wote waliitwa, wakawafuatilia Wamidiani.


Waisraeli walipotoka kuwafuatilia Wafilistini, waliteka vitu ndani ya kambi yao.


Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”


Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις