Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.
Lakini musimwasi tu Yawe, wala musiwaogope wenyeji wa inchi hiyo. Maana wao ni kama mboga tu kwetu. Kingo yao imekwisha kuondolewa kwao naye Yawe yuko pamoja nasi. Musiwaogope!
Sasa ninaomba unipe inchi hii ya milima ambayo Yawe aliniahidi siku ile. Wewe ulisikia siku ile kwamba Waanaki waliishi humo katika miji yenye kuta; labda Yawe atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza kama vile Yawe alivyosema.”
Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”
Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”