1 Samweli 16:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Samweli akafanya sawa alivyoambiwa na Yawe, akaenda Betelehemu. Wazee wa muji wakatoka kwenda kumupokea wakiwa wanatetemeka, wakamwuliza: “Umekuja kwa amani?”
Ninaamua hivyo kwa sababu ya mama yako, Rakeli. Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani yeye alikufa katika inchi ya Kanana, tukiwa karibu kufika Efurata, akaniachia huzuni. Basi, nikamuzika palepale, kando ya njia inayokwenda Efurata, maana yake Betelehemu.”
Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”
Nyuma, Adonia mwana wa Hagiti, alimwendea Batiseba, mama ya Solomono. Batiseba akamwuliza: “Unaleta habari ya amani?” Adonia akamujibu: “Ndiyo, ninaleta habari ya amani.
Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.
Halafu watu wote wa inchi ya Wagerasi wakashikwa na woga mukubwa, kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke kwao. Basi Yesu akaingia ndani ya chombo, kusudi apate kuondoka kule.