Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 15:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Tangu leo Yawe ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako na atamupa mutu mwingine kati ya wajirani zako anayekuwa bora kuliko wewe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 15:28
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe alimwapia Daudi kwamba atauhamisha ufalme kutoka jamaa ya Saulo na kumupa yeye. Naye atatawala inchi ya Israeli na Yuda kutokea Dani mpaka Beri-Seba.”


Sasa, mulilete jambo hilo mbele ya watu kwa sababu Yawe alimwahidi Daudi hivi: ‘Kwa mukono wako wewe Daudi mutumishi wangu, nitawaokoa watu wangu Waisraeli kutoka Wafilistini na kutoka waadui zao wengine.’ ”


Mungu aniue ikiwa sitatimiza yote ambayo Yawe alimwapia Daudi.


Daudi akamwambia Mikali: “Nilikuwa mbele ya Yawe ambaye alinichagua mimi pahali pa baba yako na jamaa yake, kwa kunichagua kuwa mukubwa juu ya Waisraeli, watu wa Yawe. Kwa hiyo mimi nitacheza tu mbele ya Yawe.


Kwa hiyo Yawe akamwambia Solomono: “Kwa kuwa umeamua kufanya hivyo, ukavunja agano langu nawe, na kuasi masharti yangu niliyokupa, hakika nitakunyanganya huo utawala na kumupa mutumishi wako.


pahali pa kumwendea Yawe kwa kumwomba shauri. Kwa sababu hiyo Yawe akamwua, na akamupa Daudi mwana wa Yese ufalme wake.


Anawaangamiza wenye nguvu bila uchunguzi, na kuwaweka wengine pahali pao.


Muti uliouona ukiwa mukubwa na wenye nguvu, ambao matawi yake marefu yalifika mbinguni, nao ukionekana kutoka kila pahali katika dunia,


Wakaaji wote wa dunia si kitu; anafanya anavyotaka na viumbe vya mbinguni, na wakaaji wa dunia; hakuna anayeweza kumupinga, au kusema: Unafanya nini?


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Kisha kumwondosha Saulo, Mungu akasimika Daudi kuwa mufalme wao. Na yeye mwenyewe alimushuhudia akisema: ‘Nimejichagulia Daudi mwana wa Yese, kwa maana ni mutu mwenye kunipendeza. Huyu ndiye atakayefanya mambo yote ninayotaka.’


Kila mutu anapaswa kutii wakubwa wenye mamlaka. Maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; nao wakubwa wanaotawala wamesimikwa na Mungu.


Lakini sasa ufalme wako hautadumu kwa sababu amri Yawe aliyokuamuru haukuitii. Yawe amejitafutia mutu mwingine ambaye atamutii kwa moyo wote, na huyo ndiye ambaye atamuchagua kuwa mutawala juu ya watu wake.”


Hivyo, Yese alituma mutu, naye akaletwa. Yule kijana alikuwa mwenye afya, mwenye macho yenye kungaa na wa kupendeza. Yawe akamwambia Samweli: “Sasa, huyu ndiye; simama umupakae mafuta.”


Saulo hakupendezwa na maneno ya wimbo huo. Akakasirika sana. Akasema: “Wamemupa Daudi elfu makumi, lakini mimi wamenipa maelfu tu. Linalobakia ni kumupa Daudi ufalme.”


Nyuma ya Yawe kukutendea mazuri yote aliyokuahidi, na kukuchagua kuwa mutawala wa Israeli,


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις