Elisha akamujibu: “Sikiliza neno la Yawe: Kesho kwa wakati kama huu, humu Samaria kilo tatu za unga bora wa ngano zitanunuliwa kwa kipande kimoja cha feza, na kilo sita za shayiri kwa kipande kimoja cha feza.”
Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.
Kama mukimutii Yawe na kumutumikia na kusikiliza sauti yake bila kuiasi amri yake, kama ninyi wenyewe pamoja na mufalme anayewatawala mukimufuata Yawe, Mungu wenu, basi mutafanikiwa.
Samweli akamujibu Saulo: “Umefanya kipumbafu. Haukutii mambo Yawe, Mungu wako, aliyokuamuru. Kama ungetii, Yawe angeudumisha milele ufalme wako juu ya Israeli.
“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”