Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 14:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Kulikuwa vita kali na Wafilistini kwa muda wote Saulo alipokuwa mufalme. Na kila mara Saulo alipomupata mutu mwenye nguvu au shujaa alimukamata apate kujiunga na waaskari wake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 14:52
4 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wafilistini walikuwa na magari elfu makumi tatu, waaskari elfu sita wapanda-farasi na kikundi cha waaskari wa miguu wengi kama muchanga wa bahari. Wote walipanda juu na kupiga kambi yao kule Mikimasi, upande wa mashariki wa Beti-Aweni.


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


Samweli alipokuwa muzee, aliwafanya wana wake kuwa waamuzi wa Waisraeli.


Samweli aliwaambia: “Hivi ndivyo mufalme wenu atakayewatawala atakavyowatendea: wana wenu atawafanya wakuwe waendeshaji wa magari yake, na wengine kuwa waaskari wapanda-farasi wake, na wengine watapiga mbio mbele ya magari yake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις