Lakini watu wakamwambia: “Hautakwenda. Maana, ikiwa tutakimbia, hawatajali kitu juu yetu. Ikiwa nusu yetu watakufa, hawatahangaika nasi vilevile. Lakini wewe ni wa lazima kuliko watu elfu kumi kati yetu. Kwa hiyo inafaa wewe ubaki katika muji na kutupelekea musaada ukiwa katika muji.”
Kwa ukoo wa Yuda kutatokea: watawala wa kila namna, wakubwa wenye nguvu kama jiwe kubwa la musingi, wanaokuwa imara kama musumari wa hema, wenye nguvu kama upinde wa vita.
Ninamwona atakayekuja, ninamwona, lakini hayuko karibu. Nyota itatokea kwa wazao wa Yakobo, atatokea mufalme kati ya Waisraeli. Kwa fimbo yake atapiga viongozi wa Wamoabu, atawaangamiza wazao wote wa Seti.
Na Yesu akawaambia: “Hamujasoma bado Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji limekuwa jiwe kubwa la musingi. Ni Bwana aliyefanya jambo hili, nalo ni ajabu sana kwetu.’
Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.
Kwa hiyo Waisraeli hawawezi kuwashinda waadui zao. Wanawakimbia waadui zao kwa sababu wamejifanya wenyewe kuwa kitu cha kuangamizwa! Sitakuwa pamoja nao tena musipoharibu vitu vinavyokuwa kati yenu vilivyotolewa viangamizwe.
Viongozi wote wa makabila ya Israeli wakajitokeza mbele ya mukusanyiko wa watu wa Mungu. Wote kwa jumla walikuwa waaskari elfu mia ine wa miguu wenye silaha.