1 Samweli 14:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
28 Mutu mumoja akamwambia: “Baba yako aliwaapiza watu vikali, akisema: ‘Mutu yeyote atakayekula chakula leo alaaniwe.’ ” Nao watu walikuwa wazaifu kwa ajili ya njaa.
Siku ile, Waisraeli walisumbuliwa sana maana Saulo alikuwa amewaapiza watu akisema: “Alaaniwe mutu yeyote atakayekula chakula mbele jua kutua, na mbele sijajilipiza waadui zangu kisasi.” Kwa hiyo, siku yote, hakuna mutu aliyeonja chakula chochote.
Lakini Yonatani hakusikia wakati baba yake alipowaapiza watu. Halafu akainua fimbo aliyokuwa nayo, akaichovya kwenye sega la asali, akakula asali hiyo. Hapo akajisikia kuwa na nguvu.
Kwa hiyo Saulo akamwambia Yonatani: “Uniambie jambo ulilofanya.” Yonatani akajibu: “Nilikula asali kidogo kwa kutumia fimbo yangu. Niko hapa na niko tayari kufa.”