Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Waisraeli walipoona wako katika taabu (maana walikuwa wanashambuliwa vikali), walianza kujificha. Wengine walijificha katika mapango, wengine ndani ya mashimo, wengine kwenye mawe makubwa, wengine kwenye makaburi na wengine kwenye visima.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 13:6
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Daudi akamujibu Gadi: “Nina mashaka makubwa! Lakini afazali kuazibiwa na Yawe, kuliko kutiwa katika mikono ya watu, maana yeye ana rehema sana.”


Lakini hawa ni watu walioibwa mali yao na kunyanganywa! Wote wamenaswa katika mashimo, wamefungwa katika kifungo. Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa, wamekamatwa mateka na hakuna anayesema: Muwarudishe!


Kisima ambamo Isimaeli alitupa maiti za wale watu aliowaua ni kile kikubwa ambacho mufalme Asa alikuwa amekichimba kwa kujikinga na Basha, mufalme wa Waisraeli. Isimaeli mwana wa Netania alikijaza kisima hicho maiti za wale watu aliowaua.


Uwaambie hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hao wanaokaa katika miji hiyo inayokuwa mabomoko, wataagamia kwa upanga; anayekuwa katika vijiji nitamutoa akuliwe na nyama wakali; na wale wanaokuwa kwa milima na ndani ya mapango watakufa kwa ugonjwa mukali.


Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.


Dunia haikustahili kuwa na watu kama hawa! Walitangatanga katika jangwa na katika milima, wakiishi katika mapango na mashimo ndani ya udongo.


Watu wa Ai walipoangalia nyuma, wakaona moshi ukitoka katika muji ukipanda mpaka mbinguni. Nao hawakukuwa na uwezo wa kukimbia upande wowote, maana Waisraeli waliwageukia wale waliokuwa wanawafuatilia.


Waamoni nao walivuka muto Yordani kupigana na makabila ya Yuda, Benjamina na Efuraimu. Nao Waisraeli wakapata taabu sana.


Halafu Waisraeli wakageuka kwa kupigana, na watu wa kabila la Benjamina wakashikwa na woga maana sasa waliona kwamba kuangamia kwao kulikuwa kumekaribia.


Wamidiani waliwagandamiza sana Waisraeli, mpaka wakajichimbia mashimo na mapango kwenye milima kuwa makimbilio yao.


Samweli akaondoka kutoka Gilgali na kwenda kule Gibea katika inchi ya Benjamina. Saulo alipowahesabu watu waliokuwa pamoja naye, akaona wako watu mia sita tu.


Basi, wakajitokeza kusudi Wafilistini wawaone. Wafilistini walipowaona wakasema: “Muangalie wale Waebrania wanatoka kwenye mashimo walimokuwa wamejificha.”


Hata Waisraeli wengine waliokuwa wamejificha kwenye inchi ya milima ya Efuraimu, waliposikia kwamba Wafilistini walikuwa wanakimbia, nao vilevile wakawafuatilia na kuwapiga.


Saulo alipokuwa angali kule Gibea, Wazifu wakamwendea na kumwambia: “Daudi anajificha katika inchi yetu kwenye makimbilio kule Horeshi, kwenye mulima Hakila, unaokuwa upande wa kusini wa jangwa.


Kisha Saulo aliwatwaa waaskari elfu tatu waliochaguliwa waliokuwa bora zaidi katika inchi yote ya Israeli, akaenda kumutafuta Daudi na watu wake pahali panapoitwa “Mawe ya Mbuzi wa Pori.”


Nao Waisraeli waliokuwa upande wa pili wa bonde, na wengine waliokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, naye Saulo na wana wake wamekufa, waliihama miji yao, wakakimbia. Wafilistini wakaenda na kukaa katika miji hiyo.


Wafilistini waliposikia kwamba Waisraeli wamekusanyika kule Misipa, wakubwa watano wa Wafilistini wakaenda kuwashambulia. Waisraeli waliposikia juu ya jambo lile waliwaogopa Wafilistini.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις