Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




1 Samweli 13:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wafilistini walikuwa na magari elfu makumi tatu, waaskari elfu sita wapanda-farasi na kikundi cha waaskari wa miguu wengi kama muchanga wa bahari. Wote walipanda juu na kupiga kambi yao kule Mikimasi, upande wa mashariki wa Beti-Aweni.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




1 Samweli 13:5
21 Σταυροειδείς Αναφορές  

hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao.


Shauri langu ni kwamba uwakusanye kwako watu wote wa Israeli tangia Dani mpaka Beri-Seba wakuwe wengi kama muchanga wa bahari, na wewe mwenyewe peke yako uende kwa vita.


Nao watu wa Israeli walikusanywa na kupewa silaha, wakaenda kupigana na Waaramu. Watu wa Israeli walipiga kambi, wakaonekana kama vikundi vidogovidogo vya mbuzi, lakini Waaramu walijaa katika inchi.


Sasa, ee Mungu, Yawe, utimize ahadi uliyomupa Daudi baba yangu. Umeniweka kuwa mufalme juu ya watu hawa wanaokuwa wengi kama mavumbi.


amefika katika muji wa Ayati. Amepitia kule Migoroni, mizigo yake ameiacha katika muji wa Mikimasi.


Wazao wako wangekuwa wengi kama muchanga, kama chembe za muchanga. Jina lao lisingalisahauliwa hata kidogo, wala halingalifutwa mbele yangu.


Wajane wao wamekuwa wengi kuliko muchanga wa bahari. Nao wamama wenye watoto vijana nimewaletea mwangamizaji muchana kati. Nimesababisha uchungu na vitisho viwapate kwa rafla.


Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Isaya alisema kwa sauti juu ya Waisraeli: “Ijapokuwa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaookolewa.


Basi, wakatoka wote na makundi yao makubwa ya waaskari. Nao walikuwa wengi kama muchanga wa bahari pamoja na magari mengi na farasi wengi sana.


Mupaka wake wa kaskazini ulianzia kwenye muto Yordani na kupitia upande wa kaskazini wa Yeriko na inchi ya milima ukaelekea upande wa magaribi mpaka kwenye jangwa la Beti-Aweni.


Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.


Wamidiani, Waamaleki na watu wote wa mashariki walilala katika bonde, wengi kama nzige, na ngamia wao wasiohesabika, wengi kama muchanga wa bahari.


Samweli akamwuliza: “Umefanya nini?” Saulo akamujibu: “Nilipoona watu wananiacha, na wewe haukukuja katika muda wa siku ulizosema, na tena nilipoona Wafilistini wamejipanga tayari kwa vita kule Mikimasi,


Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.


Hivyo Yawe aliwapa Waisraeli ushindi. Vita ilienea mpaka kupita Beti-Aweni.


Kulikuwa vita kali na Wafilistini kwa muda wote Saulo alipokuwa mufalme. Na kila mara Saulo alipomupata mutu mwenye nguvu au shujaa alimukamata apate kujiunga na waaskari wake.


Wafilistini walikusanya makundi yao ya waaskari kule Soko, muji unaokuwa katika inchi ya Yuda, tayari kwa vita. Walipiga kambi katika sehemu moja inayoitwa Efesi-Damimu kati ya Soko na Azeka.


Siku hiyo Wafilistini walishindwa na Yawe aliwazuia Wafilistini kuishambulia inchi ya Israeli wakati wote Samweli alipokuwa anaishi.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις